Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Shule yenye darasa moja tangu 2014
Elimu

Shule yenye darasa moja tangu 2014

Spread the love

 

BWANAHERI Akili, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi, Namalombe iliyopo Nanyumbu mkoani Mtwara, ameiomba serikali kujenga madarasa mengine katika shule yake kwa kuwa, mpaka sasa ina darasa moja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Nanyumbu … (endelea).

Amesema, darasa hilo lilijengwa mwaka 2014 lakini mpaka sasa, hakuna madarasa mengine hivyo kusababisha usumbufu kwa wanafunzi.

Ombi hilo liliongezwa mkazo na wanafunzi wa shule hiyo, wakati David Silinde, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), kufika katika shule hiyo wakati wa ziara yake, mkoani Mtwara.

Wanafunzi walimueleza Silinde kwamba, wanapata tabu kwa kufundishwa wakiwa chini ya mikorosho kutokana na kukosa madarasa kwa muda mrefu.

“Tunasomea chini ya mikorosho, tunapata tabu, tunaomba kujengewa madarasa,” wanafunzi hao walimueleza Silinde huku Mwalimu Akili akisitiza “tuna darasa moja tu tangu 2014.”

“Wanafunzi wa darasa la saba, darasa la kwanza na darasa awali wanalazimika kusoma chini ya mkorosho huku. Darasa la pili, tatu, nne, tano na sita wote wakisoma katika jengo la darasa moja lililopo, hivyo kufanya kiwango cha kufundisha kuwa kidogo huku wakitumia choo kimoja cha Nyasi wote (walimu na wanafunzi),” amesema Mwalimu Akili.

Silinde alifika katika shule hiyo, baada ya kupata taarifa kuwepo kwa shule yenye darasa moja.

Baada ya kushuhudia shule hiyo, Silinde alimwagiza Hamis Dambaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri Wilaya ya Nanyumbu, kujenga madarasa manne haraka ndani ya miezi miwili.

Pia, amemuagiza kutenga bajeti ili kujenga nyumba za walimu, ofisi na madarasa mengine huku yeye (naibu waziri) akihaidi kujenga madarasa matatu kwa kutumia mfuko wa Tamisemi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!