Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko TCRA yasitisha utoaji leseni za ‘Online’
Habari Mchanganyiko

TCRA yasitisha utoaji leseni za ‘Online’

Mhandisi Andrew Kisaka, Mkuu wa Idara ya Leseni TCRA
Spread the love

 

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imesitisha kutoa leseni mpya za maudhui ya mtandaoni (Online TV na Blogs). Anaripoti Yusuph Katimba, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI Online leo Ijumaa tarehe 5 Februari 2021, Mhandisi Andrew Kisaka ambaye ni Mkuu wa Idara ya Leseni TCRA, amesema maombi mapya ya leseni yamesitishwa kuanzia sasa.

“Leseni mpya kwa ajili ya maudhui ya mtandaoni zimesitishwa mpaka tarehe 30 Juni 2021,” amesema Kisaka.

Amefafanua, kwamba wateja wenye leseni ambao wanataka kuhuisha, wanaruhusiwa kuendelea kufanya hivyo wakati wowote.

“Kwa wale ambao wanazo leseni na wanataka kuzihuisha, hawa wanaruhusiwa. Kilichositishwa ni utoaji wa leseni mpya mpaka tarehe hiyo,” amesema.

Hata alipoulizwa sababu za mamlaka hiyo kuamua kusitisha utoaji wa leseni mpya, Kisaka amesema “tunataka kufanya tathmini ya maudhui ya mtandaoni kwa sasa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!