Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko TCRA yasitisha utoaji leseni za ‘Online’
Habari Mchanganyiko

TCRA yasitisha utoaji leseni za ‘Online’

Mhandisi Andrew Kisaka, Mkuu wa Idara ya Leseni TCRA
Spread the love

 

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imesitisha kutoa leseni mpya za maudhui ya mtandaoni (Online TV na Blogs). Anaripoti Yusuph Katimba, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI Online leo Ijumaa tarehe 5 Februari 2021, Mhandisi Andrew Kisaka ambaye ni Mkuu wa Idara ya Leseni TCRA, amesema maombi mapya ya leseni yamesitishwa kuanzia sasa.

“Leseni mpya kwa ajili ya maudhui ya mtandaoni zimesitishwa mpaka tarehe 30 Juni 2021,” amesema Kisaka.

Amefafanua, kwamba wateja wenye leseni ambao wanataka kuhuisha, wanaruhusiwa kuendelea kufanya hivyo wakati wowote.

“Kwa wale ambao wanazo leseni na wanataka kuzihuisha, hawa wanaruhusiwa. Kilichositishwa ni utoaji wa leseni mpya mpaka tarehe hiyo,” amesema.

Hata alipoulizwa sababu za mamlaka hiyo kuamua kusitisha utoaji wa leseni mpya, Kisaka amesema “tunataka kufanya tathmini ya maudhui ya mtandaoni kwa sasa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!