Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Simba yashusha viingilio mchezo dhidi ya TP Mazembe
Michezo

Simba yashusha viingilio mchezo dhidi ya TP Mazembe

Spread the love

 

UONGOZI wa klabu ya Simba umeamua kushusha viingilio kutoka Sh. 3,000 mpaka Sh. 2,000, kwenye mchezo wao dhidi ya TP Mazembe kutoka Congo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo ambao utakuwa wa mwisho kwenye michuano ya Simba Super Cup, utachezwa siku ya Jumapili tarehe 31 Januari 2021, kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam majira ya saa 10 jioni.

Hayo yamethibitishwa na Afisa habari wa klabu hiyo, Haji Manara mara baada ya kumalizika kwa mchezo kati ya Simba dhidi ya Al Hilal ambao waliibuka na ushindi wa mabao 4-1.

“Mchezo wetu dhidi ya TP Mazembe tumeamua kushusha kiingilio kutoka Sh. 3,000 hadi Sh. 2,000 na tunaomba wanasimba wajitokeze kwa wingi,” alisema Manara.

Wakati akisema hayo tayari klabu ya TP Mazembe wameshawasili nchini leo mchana kwa ajili ya michuano hiyo ambayo inatumiwa na klabu hizo kujiweka sawa kuelekea hatua ya makundi ya Ligi ya mabingwa Afrika itakayoanza tarehe 12 Februari 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!