Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Morrison ateka Show ya Simba Dar
MichezoTangulizi

Morrison ateka Show ya Simba Dar

Spread the love

 

DAKIKA tatu zilizotosha kumfanya Bernard Morisson kuibuka mchezaji bora wa mechi mara baada ya kupachika mabao mawili kwenye mchezo wa Kombe la Simba dhidi ya Al Hilal ya Sudan. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea)

Mchezo huo wa kujipima nguvu kwa ajili ya maandalizi ya michuano ya Ligi ya mabingwa ambapo Simba walifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 4-1.

Morrison ambaye aliingia dakika ya 62 ya kipindi cha pili akichukua nafasi ya Francis Kahata ambapo ilimchukua dakika 25 akiwa uwanjani kupachika bao lake la kwanza dakika ya 87, na dakika tatu baadae akapicha bao la pili ambalo lilikuwa bao la nne kwenye mchezo huo dakika ya 90.

Morrison hakuonekana uwanjani muda mrefu kutokana na kusumbuliwa na majeraha toka mwezi wa 12 mwaka jana.

 

Mara baada ya mchezo huo kocha mkuu wa klabu ya Simba, Didier Gomes alimuelezea mchezaji huyo kuwa anakipaji cha hali ya juu ila anahitaji kuwa fiti ili aweze kucheza mara kwa mara.

“Morrison ni mchezaji mzuri anahitaji kucheza muda mrefu, ameonesha kiwango kizuri anahitaji kuwa fiti kwa utimamu wa mwili kwa kuwa ni kitu muhimu” alisema Gomes.

Baada ya kupata matokeo hayo Simba itashuka tena dimbani siku ya Jumapili ambapo watavaana na TP Mazembe kwenye mchezo wa pili wamichuano hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

error: Content is protected !!