AFISA Habari na Mawasiliano wa klabu ya Yanga, Hassan Bumbuli amefungiwa miaka mitatu kujihusisha na masuala ya mpira wa miguu baada ya kushindwa kulipa faini ya Sh. 5,000,000. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Tarehe 28 Septemba 2021, Hassan Bumbuli alitakiwa kulipa kiasi hiko cha fedha baada ya kukutwa na hatia kwenye Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na kutotakiwa kufanya kosa la kimaadili katika kipindi cha miaka miwili lakini mambo yote hayakutekelezwa.
Taarifa ya kufungiwa Bumbuli imetolewa hii leo tarehe 27 Januari 2021 huku ikieleza kuwa adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia kifungu cha 73 (8)(a) cha maadili ya TFF toleo la 2013.
Leave a comment