Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Uchaguzi Mkuu Uganda: Sanduku la kura laibwa
Kimataifa

Uchaguzi Mkuu Uganda: Sanduku la kura laibwa

Bobi Wine
Spread the love

VITUKO vya Uchaguzi Mkuu nchini Uganda vinaanza kudhihiri, tayari sanduku moja la kura linaripotiwa kuibwa na kutokomea kusikojulikana. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Wizi wa sanduku hilo umethibitishwa na Paul Bukenya, Msemaji wa Tume ya Uchaguzi nchini humo akieleza, sanduku hilo limeibwa likiwa na kura ndani yake.

Bukenya amesema, wizi wa sanduku hilo umetokea katika eneo la Rushenyi, Ntungano ambapo ni mashariki mwa nchini na kuwa, hajulikani mtu ama watu waliohusika kwenye wizi huo.

Amesema, tayari taarifa za wizi huo zimewasilishwa kwa tume pamoja na kwa Jeshi la Polisi ambalo sasa linaendesha msako mkali.

Hata hivyo, Bukenya amesema tukio hilo ni la bahati mbaya “tukio hili ni la bahati mbaya, kwa sasa tunalishughulikia na kisha tutatoa taarifa.”

Leo tarehe 14 Januari 2021, Raia wa Uganda wanapiga kura kumchagua rais wa nchi hiyo, Rais Museveni anakabiliana na upinzani mkali kutoka kwa Robert Kyagulanyi (Bobi Wine) (38), wanamuziki wa kizazi kipya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!