Friday , 29 March 2024
Habari za Siasa

CCM wabanana mbavu

Mizengo Pinda, Waziri Mkuu Mstaafu
Spread the love

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Iringa kimetengeneza utaratibu mpya wa kuwapima madiwani na wabunge wake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa … (endelea).

Sasa mbunge na diwani kwenye mkoa huo, atatakiwa kukutana na wananchi kila baada ya miezi mitatu na kueleza nini amefanya kwenye kipindi hicho.

Uamuzi huo umefikiwa kwenye kikao maalumu cha chama hicho kilichowakutanisha wabunge na madiwani hao ambapo Dk. Abel Nyamahanga, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa amesema “itasaidia kufuatilia ahadi zao.”

Dk. Nyamahanga amesema, chama hichi kimeweka utaratibu huo kuwalazimisha viongozi hao kutoa taarifa lakini pia kuonesha mafanikio ya uchapaji kazi wao.

Amesema, hatua hiyo pia itaongeza imani ya wananchi kwa CCM na kurahisisha uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kwa chama hicho.

Kikao hichi pia kimehudhuriwa na Mizengo Pinda, Waziri Mkuu Mstaafu ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa.

Pinda amewataka wabunge na madiwani hao kuwa karbu na wananchi ili kujua changamoto zinaqzowakabilia na kujua namna ya kuzitatua.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!