Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Michezo TFF yaja na Bonanza la Waandishi
Michezo

TFF yaja na Bonanza la Waandishi

Boniface Wambura, Mkuu wa Habari na Masoko wa TFF
Spread the love

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeandaa bonanza kwa ajili ya vyombo vya Habari litakalofanyika tarehe 6 Desemba 2020 kwenye viwanja vya Leaders Club vilivyopo Kinondoni Jijini Dar es Salaam. Anaripoti Kewlvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Bonaza hilo ambalo litajulikana kwa jina la TFF Media Day likiwa na lengo la kukutanisha waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini na kujumuika pamoja katika kuumaliza mwaka.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Masoko wa TFF, Boniface Wambura amesema lengo la bonaza hilo ni kutambua na kuthamini mchango wa vyombo vya habari kataka maendeleo ya mpira wa miguu nchini.

“Vyombo vya habari ni moja ya wadau wetu wakubwa katika kutangaza na kufahamisha wadau wa mpira wa miguu kuhusu TFF, nini tunataka kufanya na pia tutatumia muda huo kukutana na waandishi pamoja na viongozi wa TFF nje ya maeneo ya kazi,” alisema Wambura.

Aidha Wambura aliongezea, Bonanza hilo halitaishia mwaka huu bali litakuwa ni tukio litakalofanyika kila mwaka ila huu utakuwa ni mwanzo tu.

Jambo hili litakuwa ni mara ya kwanza kwa Taasisi hiyo ya juu kwenye mpira wa miguu nchini kuandaa siku kwa ajili ya vyombo vya habari ambayo itakuwa inashirikisha michezo mbalimbali huku lengo likiwa ni kufahamia Zaidi nje ya mazingira ya kazi.

Bonanza hilo ambalo litaanza majira ya saa 3 asubuhi mpaka saa 12 jioni litakuwa na michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, mziki pamoja na mchezo wa kuvuta kamba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Idris Sultan anogesha msimu wa 3 wa Bridgerton

Spread the loveSTAA wa burudani kutoka ardhi ya Tanzania, Idris Sultan amenogesha...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

error: Content is protected !!