Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM yajikusanyia wabunge, wapinzani wapata 2
Habari za Siasa

CCM yajikusanyia wabunge, wapinzani wapata 2

Shamsia Mtamba
Spread the love

MATOKEO ya Uchaguzi Mkuu nchini Tanzania uliofanyika Jumatano iliyopita tarehe 28 Oktoba 2020 yanaonyesha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimejikusanyia viti vingi vya udiwani na ubunge. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Hadi kufikia saa 7 mchana, matokeo hayo yanayotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) yanaonyesha CCM imekwisha kujikusanyia majimbo 220 kati ya 264.

Chadema ina mbunge mmoja, Aida Khenan wa Nkasi Kaskazini ambaye amemuangusha mbunge wa CCM aliyekuwa anaongoza jimbo hilo kwa miaka kumi mfululizo Ally Kessy.

Aida Khenan

Jimbo jingine ambalo upinzani wamejikusanyia ni la Mtwara Vijijini ambalo Shamsia Mtamba wa CUF amemuangusha mbunge wa CCM aliyekuwa anatetea jimbo hilo, Hawa Ghasia.

Shamsia Mtamba

Katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka 2015, kati ya majimbo 264, upinzani walijikusanyia majimbo zaidi ya 65 lakini mpaka sasa, majimbo yaliyosalia kutangazwa ni 45 pekee.

Endelea kufuatilia mitandao yetu kwa habari na taarifa mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!