Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM yajikusanyia wabunge, wapinzani wapata 2
Habari za Siasa

CCM yajikusanyia wabunge, wapinzani wapata 2

Shamsia Mtamba
Spread the love

MATOKEO ya Uchaguzi Mkuu nchini Tanzania uliofanyika Jumatano iliyopita tarehe 28 Oktoba 2020 yanaonyesha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimejikusanyia viti vingi vya udiwani na ubunge. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Hadi kufikia saa 7 mchana, matokeo hayo yanayotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) yanaonyesha CCM imekwisha kujikusanyia majimbo 220 kati ya 264.

Chadema ina mbunge mmoja, Aida Khenan wa Nkasi Kaskazini ambaye amemuangusha mbunge wa CCM aliyekuwa anaongoza jimbo hilo kwa miaka kumi mfululizo Ally Kessy.

Aida Khenan

Jimbo jingine ambalo upinzani wamejikusanyia ni la Mtwara Vijijini ambalo Shamsia Mtamba wa CUF amemuangusha mbunge wa CCM aliyekuwa anatetea jimbo hilo, Hawa Ghasia.

Shamsia Mtamba

Katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka 2015, kati ya majimbo 264, upinzani walijikusanyia majimbo zaidi ya 65 lakini mpaka sasa, majimbo yaliyosalia kutangazwa ni 45 pekee.

Endelea kufuatilia mitandao yetu kwa habari na taarifa mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!