Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa CCM yajikusanyia wabunge, wapinzani wapata 2
Habari za Siasa

CCM yajikusanyia wabunge, wapinzani wapata 2

Shamsia Mtamba
Spread the love

MATOKEO ya Uchaguzi Mkuu nchini Tanzania uliofanyika Jumatano iliyopita tarehe 28 Oktoba 2020 yanaonyesha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimejikusanyia viti vingi vya udiwani na ubunge. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Hadi kufikia saa 7 mchana, matokeo hayo yanayotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) yanaonyesha CCM imekwisha kujikusanyia majimbo 220 kati ya 264.

Chadema ina mbunge mmoja, Aida Khenan wa Nkasi Kaskazini ambaye amemuangusha mbunge wa CCM aliyekuwa anaongoza jimbo hilo kwa miaka kumi mfululizo Ally Kessy.

Aida Khenan

Jimbo jingine ambalo upinzani wamejikusanyia ni la Mtwara Vijijini ambalo Shamsia Mtamba wa CUF amemuangusha mbunge wa CCM aliyekuwa anatetea jimbo hilo, Hawa Ghasia.

Shamsia Mtamba

Katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka 2015, kati ya majimbo 264, upinzani walijikusanyia majimbo zaidi ya 65 lakini mpaka sasa, majimbo yaliyosalia kutangazwa ni 45 pekee.

Endelea kufuatilia mitandao yetu kwa habari na taarifa mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!