Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yaipiku CCM wagombea ubunge wanawake
Habari za Siasa

Chadema yaipiku CCM wagombea ubunge wanawake

Spread the love

VYAMA vya siasa nchini Tanzania, vimefanya uteuzi wa wagombea ubunge katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 huku idadi ya wanawake ikiwa hairidhishi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea)

Chama Cha Mapinduzi (CCM), Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Chama Cha Wananchi (CUF) na ACT-Wazalendo vimekwisha kamilisha uteuzi wa wagombea wao wa ubunge wa majimbo.

Jumla ya majimbo 264 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yatahusika kwenye uchaguzi mkuu kwa maana ya majimbo 214 ya Tanzania Bara na 50 Zanzibar.

Rais John Magufuli, Mwenyekiti wa CCM

Katika uteuzi uliofanywa na Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapindizi (CCM), kwenye majimbo 264, imeteua wanawake wasiozidi 25 kugombea kwenye majimbo.

Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania cha Chadema, katika majimbo 264 ya uchaguzi, ina wagombea wanawake zaidi ya 50.

Soma zaidi hapa

Sera kabambe ya wanawake, wenye ulemavu na vijana yaandaliwa

Chama cha Wananchi (CUF), katika uteuzi uliotolewa leo Jumatatu kwenye majimbo 136 ya Tanzania Bara, imeteua wanawake zaidi ya 30 kusimama majimboni.

ACT-Wazalendo ina wagombea zaidi ya 20.

Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha), Halima Mdee akizungumza katika Mkutano Mkuu wa chama hicho mwezi uliopita, alisema wamejipanga kuhakikisha wanatoa ushindani mkubwa majimboni.

Mdee ambaye anagombea ubunge Kawe jijini Dar es Salaam alisema, wanawake ni jeshi kubwa, wakiaminiwa wanaweza kufanya mapinduzi na wamekuwa na msimamo wa kutotohama hama.

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema

Mwishoni mwa wiki, Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), Hebron Mwakagenda alisema ushiriki wa wanawake, vijana na wenye ulemavu umekuwa hauridhishi.

Alisema, kutokana na hilo, Jukata kwa kushirikiana na Ushiriki Tanzania wanaandaa sera ya kitaifa ya ushiriki wa makundi hayo kwenye siasa ili kuwapo na uwiano sawa.

Mwakagenda alisema, wanawake hawapewi kipaumbele kwenye majimbo badala yake wanaelezwa wasubiri kugombea viti maalum jambo ambalo linaleta shida, hivyo vyama vya siasa vinapaswa kutoa haki sawa kwa wanaume na wanawake.

Alisema, sera hiyo iliyokusanya maoni ya wadau mbalimbali, itakapokamilika itawasilishwa serikalini kwa utekelezaji ili kuwezesha kufikia ile 50 kwa 50.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!