Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto: Mnazo sababu za kuing’oa CCM
Habari za Siasa

Zitto: Mnazo sababu za kuing’oa CCM

Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo
Spread the love

ZITTO Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo amewaeleza wanachama wa chama hicho Tunduru, Mtwara kwamba wanayo sababu ya kuing’oa CCM madarakani. Anaripoti Faki Sosi, Tunduru … (endelea).

Akizungumza kwenye mkutano wa ndani na wachama wa chama hicho tarehe 22 Julai 2020, Zitto aliye kwenye ziara ya kichama na baadhi ya viongozi wa chama hicho mkoani Mtwara amesema, safari hii ‘lazima kieleweke.’

Kwenye kikao hicho, Zitto amewapa mfano wa namna mikutano ya kisiasa ilivyozuiliwa huku akisitiza, Uhuru wa kujieleza miongoni mwa Watanzania umetoweka kutokana na hofu iliyojengwa na Serikali ya Awamu ya Tano.

“Mikutano ilikuwa ni jambo la kawaida, kila chama kilikuwa na haki ya kufanya mikutano, leo hii hata kufanya mikutano ya ndani difenda za polisi zinazunguka.

“Miaka 13 iliyopita nilikuja Tunduru, tunafanya mikutano ya hadhara na watu wa vyama vyote wanahudhuria na wanasikiliza. Sasa hivi, watu wanaogopa kuja kusikiliza, kwa sababu polisi bila sababu zozote wanazunguka na madifenda,” amesema Zitto.

https://www.youtube.com/watch?v=rp7LlTWnQAU

Kutokana na aliyoieleza Zitto, amesema kuna kila sababu ya kuiondoa Serikali inayotokana na CCM kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 28 Oktoba 2020.

“Serikali ya Chama Cha Mapinduzi inapaswa kuondolewa madarakani kwa sababu inaminya haki zenu. Uhuru wenu wa mawazo, Uhuru wenu wa kujieleza, Uhuru wenu wa kuchanganyika, Uhuru wenu wa kukosoa serikali au kusifia serikali umetoweka.

“Leo hii watu hawana Uhuru, ukiongea kitu kuhusu serikali, unajitazama. Sisi 2020 tunazungumzia Uhuru, tumerudi nyuma hatujarudi nyuma?” alipohoji hivyo alijibiwa “tumerudi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!