Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto: Mnazo sababu za kuing’oa CCM
Habari za Siasa

Zitto: Mnazo sababu za kuing’oa CCM

Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo
Spread the love

ZITTO Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo amewaeleza wanachama wa chama hicho Tunduru, Mtwara kwamba wanayo sababu ya kuing’oa CCM madarakani. Anaripoti Faki Sosi, Tunduru … (endelea).

Akizungumza kwenye mkutano wa ndani na wachama wa chama hicho tarehe 22 Julai 2020, Zitto aliye kwenye ziara ya kichama na baadhi ya viongozi wa chama hicho mkoani Mtwara amesema, safari hii ‘lazima kieleweke.’

Kwenye kikao hicho, Zitto amewapa mfano wa namna mikutano ya kisiasa ilivyozuiliwa huku akisitiza, Uhuru wa kujieleza miongoni mwa Watanzania umetoweka kutokana na hofu iliyojengwa na Serikali ya Awamu ya Tano.

“Mikutano ilikuwa ni jambo la kawaida, kila chama kilikuwa na haki ya kufanya mikutano, leo hii hata kufanya mikutano ya ndani difenda za polisi zinazunguka.

“Miaka 13 iliyopita nilikuja Tunduru, tunafanya mikutano ya hadhara na watu wa vyama vyote wanahudhuria na wanasikiliza. Sasa hivi, watu wanaogopa kuja kusikiliza, kwa sababu polisi bila sababu zozote wanazunguka na madifenda,” amesema Zitto.

https://www.youtube.com/watch?v=rp7LlTWnQAU

Kutokana na aliyoieleza Zitto, amesema kuna kila sababu ya kuiondoa Serikali inayotokana na CCM kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 28 Oktoba 2020.

“Serikali ya Chama Cha Mapinduzi inapaswa kuondolewa madarakani kwa sababu inaminya haki zenu. Uhuru wenu wa mawazo, Uhuru wenu wa kujieleza, Uhuru wenu wa kuchanganyika, Uhuru wenu wa kukosoa serikali au kusifia serikali umetoweka.

“Leo hii watu hawana Uhuru, ukiongea kitu kuhusu serikali, unajitazama. Sisi 2020 tunazungumzia Uhuru, tumerudi nyuma hatujarudi nyuma?” alipohoji hivyo alijibiwa “tumerudi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!