Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Urais NCCR-Mageuzi: Aboubakar achukua fomu, asema ndoto yake imetimia
Habari za Siasa

Urais NCCR-Mageuzi: Aboubakar achukua fomu, asema ndoto yake imetimia

Spread the love

ABOUBAKAR Juma Aboubakar leo Jumamosi tarehe 18 Julai 2020 amechukua fomu kuomba ridhaa ya Chama cha NCCR-Mageuzi, kugombea Urais wa Tanzania, katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam.

Aboubakar amekabidhiwa fomu hiyo na Anthony Komu, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya NCCR-Mageuzi, kwenye Ofisi za Makao Makuu ya chama hicho, Ilala jijini Dar es Salaam.

Baada ya kukabidhiwa fomu hiyo, Aboubakar amesema, ameamua kutia nia kugombea nafasi hiyo, ili apate fursa ya kuwaongoza Watanzania, katika misingi ya utu, maadili, umoja na udugu kama itikadi ya NCCR-Mageuzi inavyoelekeza.

Mwanasiasa huyo amesema, safari ya kusaka nafasi ya kugomnea Urais wa Tanzania aliianza miaka 28 iliyopita, hivyo anaamini NCCR-Mageuzi kitakamilisha safari yake hiyo kwa kumpitisha kuwa mgombea wake.

“Niliianza safari hii kwa muda wa miaka 28, kila siku nilikua msindikizaji. Lakini leo natia nia kugombea urais wa Tanzania ili niwe mtumishi wa Watanzania wote bara na Zanzibar na wa rika zote,” amesema Aboubakar.
Amesema yeye ni Mtanzania mwenye asili ya Zanzibar aliyezaliwa Lushoto Mkoa wa Tanga na makazi yake yote yapo Ilala jijini Dar es Salaam.

Aboubakar amesema anaona Katiba ya Tanzania inamsuta “na nimeifanyia nini Tanzania wakati nikiona wengine wametupwa nje ya mfumo wa kijamii, kisiasa na kielimu” nah ii ndiyo imenisukuma kujitokeza kuwania uongozi huu.

Naye Komu amesema, chama hicho kiko tayari kutoa ushirikiano kama atafanikiwa kushinda mchakato wa uteuzi ndani ya NCCR-Mageuzi.

“Mimi kama mwenyekiti, nimwambie sisi tuko tayari kukuunga mkono kwenye nia yako nzuri na kukupa kila aina ya ushirikiano katika kufanikisha nia hii nzuri, na hiyo itakua kamili zaidi utakapofanikiwa kuwa mgombea kwa tiketi ya chama chetu kama ukijaaliwa,” amesema Komu.

Mwenyekiti huyo wa Uchaguzi NCCR-Mageuzi, amemtaka mti ni huyo kusoma vyema katiba ya chama hicho, ili imuongoze katika harakati zake hizo.

“Uchaguzi ni jambo kubwa linaweza amua mustakabali wa maisha yetu au iendelee kuwa na amani na utulivu tunaoupenda au tuingie kwenye historia nyingine ya mfarakano, nikuombe sana chama chetu kina itikadi, tuna katiba, kanuni na mambo mengine,” amesema Komu na kuongeza.

“Itikadi yetu ni ya utu kwa mujibu wa katiba ya chama inasema, itikadi ya chama ni utu ambayo msingi yake undugu, maadili, usawa, haki, imani, mabadiliko, uhuru, wajibu, asili, kazi na endelezo. Hizi ni dhana pana sana, sasa wajibu wetu kujifunza na kuzielewa kisha kuzitekeleza,” amesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!