Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Muuguzi ajitosa ubunge Singida
Habari za Siasa

Muuguzi ajitosa ubunge Singida

Ukende William Shalla akikabidhiwa fomu ya kugombea ubunge viti maalum kupitia Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Singida na Katibu wa umoja huo mkoani humo, Edina Kugulu.
Spread the love

UKENDE William Shalla, amechukua na kurejesha fomu ya kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kugombea ubunge Viti Maalum mkoani Singida. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Shalla ambaye ni mtaalamu wa tiba ya uuguzi na ukunga, amerejesha fomu hiyo jana Jumatano tarehe 15 Julai 2020, katika Ofisi za CCM mkoa wa Singida, ambapo ilipokelewa na Edina Kugulu, Katibu wa Umoja wa Wanawate Tanzania (UWT), mkoani Singida

Mwanasiasa huyo alichukua fomu hiyo tarehe 14 Julai 2020, ambapo ametia nia kugombea ubunge Viti Maalum kupitia kundi la wanawake.

Akizungumza baada ya kurejesha fomu hiyo, Shalla alisema, ameamua kugombea nafasi hiyo ili akawawakilishe wanawake bungemi, ikiwemo kueleza changamoto zao.

CCM ilifungua zoezi la uchukuaji na urejeshaji fomu za kugombea nafasi ya ubunge, uwakilishi, udiwani na nafasi za viti maalum, tarehe 14 Julai 2020.

Kwa mujibu wa ratiba ya CCM, zoezi hilo linatarajiwa kufungwa kesho Ijumaa tarehe 17 Julai 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!