Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM wafurika kuchukua fomu za Ubunge Moshi Mjini
Habari za Siasa

CCM wafurika kuchukua fomu za Ubunge Moshi Mjini

Mkurugenzi wa Ibraline Foundation , Ibrahim Shayo akiingia kwenye gari mara baada ya kuchukua fomu ya kugombea ubunge jimbo la Moshi mjini katika ofisi za Chama cha Mapinduzi(CCM)
Spread the love

MAKADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jimbo la Moshi Mjini wamefurika kwenye ofisi ya chama hicho wilaya kuchukua fomu za kuomba kuteuliwa kugombea ubunge. Anaandika Mwandishi Wetu, Kilimanjaro…(endelea).

Leo tarehe 14 Julai 2020, ni siku ya kwanza kwa watia nia wa CCM kuchukua fomu za kuomba kupitishwa na chama hicho, zoezi hilo linatarajiwa kuhitimishwa tarehe 17 Julai 2020.

Mpaka kufika saa 8 mchana wa leo, jumla ya makada saba walikuwa tayari wamechukua fomu huku taarifa zikieleza, wengine wapo njiani kujitokeza.

Waliochukua fomu mpaka sasa ni Mkurugenzi wa Ibraline Foundation na Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa Mkoa wa Kilimanjaro, Ibrahim Shayo.

Wengine ni Priscus Tarimo, Issah Wilium, Noel Nko, Mwalimu Evans Mghase, Faraji Swai na Alfa Kiwango. Kwa leo, zoezi hilo linatarajiwa kuhitimishwa saa 12:00 jioni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!