Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Iddi Azzan: Nilitaka kujiua
Habari za Siasa

Iddi Azzan: Nilitaka kujiua

Spread the love

KASHFA ya dawa za kulevya niliyobebeshwa, ilitaka kunipelekea kufanya uamuzi wa kujitoa roho. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Ni kauli ya Iddi Azzani, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kinondoni kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), alipozungumza na MwanaHALISI Online.

Tuhuma za Azzan kujihusisha na dawa za kulevya, ziliibuka mwaka 2013 na miaka miwili baadaye, tuhuma hizo zilishika hatamu wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu 2015, yeye akiwa miongoni mwa wagombea wa Jimbo la Kinondoni.

“Tuhuma hizo ziliniathiri sana pamoja na familia yangu, hasa watu niliokuwa nawaongoza, zilitoka mwaka 2013, baadhi ya mitandao na magazeti yalitumika kuandika tuhuma hizo, na zilizidi mwaka 2015. Kwa kweli zimeniathiri sana kisaikolojia mpaka sasa.

“Nilifikia mahali pabaya, jinsi nilivyo na heshima niliyonayo na audilifu wangu, halafu jambo hilo linatoka na linalazimishwa lionekane ni kweli, ilifika mahali nilisema bora nife, bora nijipige risasi nife ila familia yangu ilifanya kazi ya ziada,” amesema Azzan.

Pia mwaka 2017, Paul Makonda ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alipoanza kampeni ya kutokomeza biashara ya uuzaji, usambazaji na utumiaji wa dawa za kulevya, jina la Azzan lilikuwa miongoni mwayo.

“Ningeshangaa kama nisingetajwa. Niliitwa polisi kuhusu tuhuma hizo, nilikaa siku nne huku uchunguzi ukifanywa kuthibitisha kama nahusika ama la! Baada ya siku nne niliachwa kwa kuwa hawakuona chochote kinachonihusisha na tuhuma hizo,” amesema.

“Na mimi nigeshangaa sana Makonda kama angetaja watu wote halafu mimi asinitaje, ningeona ni adui yangu. Kwa bahati nzuri naye akanitaja na nilitii amri yake ya kwenda polisi, sikwenda na wanasheria wala ndugu yanu,” amesema Azzan.

Azan amesema, alitumia nguvu nyingi kujisafisha dhidi ya tuhuma hizo, licha ya kwamba katika hali ya kawaida, zimeacha kovu, kwa kuwa tuhuma huwa hazifutiki.

Katika harakati zake za kujisafisha, Azzan amesema alijisalimisha polisi na hata kwenda katika Shirika la Polisi la Kimaraifa (Interpol), ili wachunguze juu ya tuhuma hizo, kwa minajili ya kumchukulia hatua kama anahusika au kumsafisha kama ahusiki nazo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!