Saturday , 2 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Mauaji ya watu 166 Ethiopia
Kimataifa

Mauaji ya watu 166 Ethiopia

Spread the love

JESHI la Polisi nchini Ethiopia, limethibitisha mauaji ya watu 166, raia wa taifa hilo kwenye maandamano ya kulaani mauaji ya mwanamuziki Haacaaluu Hundeessa. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

“Mauaji ya watu 166 yametokea kwenye maandamano yanayofanywa na waandamanaji kutokana na kifo cha Haacaaluu Hundeessa.

“Kutokana na kifo hicho, raia 145 na polisi 11 wamepoteza maisha. Jumla yake ni 166, wengine 10 wameuawa katika Jiji la Addis Ababa,” amefafanua Girma Gelam, Kaimu Mkuu wa Polisi katika Mji wa Oromia.

Girma amesema, watu 167 wana majeraha mabaya na kwamba watu 1,084 wamekamatwa na polisi kwa kujihusisha na maandamano hayo.

Haacaaluu ambaye ni mwanamuziki maarufu wa miondoko ya Pop, kutoka kabila kubwa kuliko yote nchini humo la Oromo, alipigwa risasi na kuuawa na watu wasiojulikana usiku wa Jumatatu wiki iliyopita.

Mauaji hayo yameibua hisia za kikabila na kutishia mwendelezo wa demokrasia iliyoanza kuchipua. Mpaka sasa, watu watano wamekamatwa wakihusishwa na mauaji hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

Kimataifa

Mateka wa Israel, Gaza kuanza kuachiwa leo

Spread the loveMakubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na vikosi vya...

Kimataifa

Israel, Hamas kusitisha mapigano kwa muda

Spread the loveNCHI ya Israel, pamoja na kikundi cha wanamgambo wa kiislamu,...

error: Content is protected !!