Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanzania yafika uchumi wa kati
Habari Mchanganyiko

Tanzania yafika uchumi wa kati

Spread the love

BENKI ya Dunia (WB) imeitangaza Tanzania kuingia katika nchi za uchumi wa kipato cha kati. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hatua hiyo imefikiwa miaka mitano kabla ya lengo la Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 inayobainisha kufikia mwaka huo, Tanzania itafikia uchumi wa kati.

Leo Jumatano tarehe 1 Julai 2020, Rais wa Tanzania, John Magufuli ametumia akaunti yake ya Twitter kutoa pongeza kwa Watanzania kwa kufikia hatua hiyo.

Rais John Magufuli

Rais Magufuli amesema, “Benki ya Dunia leo tarehe 01 Julai, 2020 imeitangaza Tanzania kuingia uchumi wa kati.”

“Nawapongeza Watanzania wenzangu kwa mafanikio haya. Huu ni ushindi mkubwa na kazi kubwa tumeifanya, tulipanga kuingia uchumi wa kati ifikapo 2025 lakini tumefanikiwa 2020. Mungi Ibariki Tanzania,” amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari Mchanganyiko

Tanzania  yasisitiza kuwa Kituo Kikuu cha Uchimbaji Madini Afrika

Spread the loveTanzania imeendelea kusisitiza adhma yake ya kuwa kituo kikuu cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

error: Content is protected !!