Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maharagande ajitosa rasmi ubunge Segerea
Habari za Siasa

Maharagande ajitosa rasmi ubunge Segerea

Spread the love

MBARALA Maharagande, Katibu wa Idara ya Haki za Binadamu Taifa wa Chama cha ACT-Wazalendo, amechukua fomu ya kugombea ubunge wa Segerea jijini Dar es Salaam, katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Maharagande amekabidhiwa fomu hiyo leo Jumatano tarehe 1 Julai 2020 na Athuman Maarufu, Katibu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Jimbo Segerea.

Baada ya kukabidhiwa fomu hiyo, Maharagande amesema, ameanza rasmi safari ya kuliwania jimbo hilo lililokuwa mikononi mwa Chama cha Mapinduzi (CCM), chini ya Bonah Kamoli.

“Safari imeanza rasmi, leo nimechukua fomu ya kugombea ubunge wa Jimbo la Segerea katika mchakato ndani ya chama,” amesema Maharagande.

 Chama cha ACT-Wazalendo kimefungua rasmi pazia la uchukuaji na urejeshaji fomu za kugombea urais ubunge, uwakilishi na udiwani leo, ambapo linatarajia kukoma tarehe 13 Julai mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!