Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msanii Vitalis Maembe ajiunga ACT-Wazalendo, atangaza kugombea Bagamoyo
Habari za Siasa

Msanii Vitalis Maembe ajiunga ACT-Wazalendo, atangaza kugombea Bagamoyo

Spread the love

VITALIS Maembe, Mwanamuziki na Mwanaharakati nchini Tanzania, amesema amejiunga na Chama cha ACT-Wazalendo kwa kuwa chama hicho kina misingi ya  kudai haki  na kujipambanua kwenye ujamaa. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Maembe  amejiunga na chama hicho leo Jumatatu tarehe 29 Juni 2020 na kukabidhiwa kadi na Ado Shaibu, Katibu Mkuu wa chama hicho, makao makuu ya ACT-Wazalendo, Makumbusho jijini Dar es Salaam.

Maembe amesema ACT-Wazalendo ni chama chenye sifa anazozihitaji kama vile yeye anavyojipambanua kwenye muziki wake.

Amesema chama hicho kimejipambanua kwenye mapambano ya haki na kutetea wanyonge na kujenga umoja wa Afrika.

Kwa upande wake, Shaibu wakati anampokea Maembe amesema, mwanamziki huyo alijipambanua kwenye mtandao kuwa anahitaji kuendeleza mapambano ya haki kupitia siasa.

Wakati huo huo, Maembe amesema kuwa endapo chama hicho kitampa ridhaa atagombea ubunge Bagamoyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!