MAHMOUD Mousavi-Majd, Raia wa Iran aliyesaidia Intelejensia ya Marekani (CIA) kumuua kamanda wa ngazi ya juu wa Iran, Qassem Soleimani amehukumiwa kunyongwa hadi kufa. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).
Januari 3 mwaka huu, ndege zisizo na rubani za Marekani nchini Iraq, zilimuua Kamanda Soleimani. Serikali ya Washington ilimlaumu Soleimani kwamba ndiye aliyekuwa akipanga mashambulizi kwenye kambi zake katika ardhi ya Iraq.
“Mahmoud Mousavi-Majd, mmoja kati ya watu walioisaidia the CIA, amekutwa na hatia na amehukumiwa kunyongwa mpaka kufa. Huyu ndio alikokuwa akiwapa taarifa maadui zetu kuhusu kamanda Soleimani.
“Majd aliwapa taarifa intelejensia ya Israel na Marekani taarifa zote za jeshi la Iran.” amesema Gholamhossein Esmaili, msemaji wa mahakama kuu nchini humo na kwamba, Majd’s atanyongwa katika siku za karibuni
Hata hivyo, taarifa ya baadaye iliyotolewa na mahakama hiyo ilidai kwamba, kunyongwa kwa Majd hakuna uhusiano na ushirikiano wake na CIA.
“Kesi kuhusu tuhuma za ukuwadi zilianza kabla ya kuuawa kwa Soleimani,” taarifa ya mahakama ilieleza hivyo. Majd alikamatwa Oktoba 2018.
Mwaka 209, Iran ilitangaza kwamba, kuna maofisa wake 17 wamekuwa wakifanya kazi na CIA, na kueleza miongoni mwao watanyongwa.
Kuuawa kwa Soleimani kulieleza kufikia kilele cha mgogoro kati ya Marekani na Iran. Iran iliamua kushambulia kambi za Marekani zilizokuwepo Iraq.
Leave a comment