Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Upinzani Tanzania: Viongozi wakuu washtakiwe kwa wanayotenda
Habari za Siasa

Upinzani Tanzania: Viongozi wakuu washtakiwe kwa wanayotenda

Salome Makamba
Spread the love

KAMBI Rasmi ya Upinzani Bungeni nchini Tanzania, imekosoa marekebisho yanayokusudiwa kufanywa katika Sheria ya Utekelezaji wa Haki na Wajibu wa Msingi, Sura ya 3 kuwa haina tija kwa Taifa na unawalenga watu fulani.
 Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Hayo yamesemwa leo Jumatano tarehe 10 Juni 2020 na Msemaji MKuu wa Kambi hiyo katika Wizara ya Katiba na Sheria, Salome Makamba wakati akiwasilisha maoni juu ya Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na.3) wa Mwaka 2020.

Katika muswada huo uliowasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Profesa Adelardus Kilangi ukipendekeza kufanyika marekebisho ya sheria 13.

Profesa Kilangi amesema, Muswada unalenga kufanya marekebisho katika Kifungu cha 4 ili kuweka masharti yatakayotaka mtu yoyote anayekusudia kufungua shauri lolote la kikatiba chini ya Ibara za 12-29 zinazohusu haki za msingi kuidhihirishia mahakama ni kwa kiasi gani mlalamikaji ameathiriwa na ukiukwaji wa haki anayolalamikia.

Amesema, marekebisho katika kifungu hiko yanapendekeza mashauri yote ya madai dhidi ya viongozi wakuu wa nchi yafunguliwe dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Lengo la marekebisho haya ni kukidhi maudhui ya dhana ya kinga ya mashtaka dhidi ya viongozi hao.

Hata hivyo, upinzani kupitia kwa Makamba umepinga marekebisho hayo akisema, “Ni muhimu Bunge hili tukufu liweze kutofautisha kati ya uvunjifu wa Ibara ya Katiba na uvunjifu wa haki za msingi za Kikatiba.”

“Uvunjifu wa ibara ya Katiba unaweza kupingwa na kila mtu kwa kuwa unahusu ulinzi wa Katiba na uvunjifu wa haki za msingi unaweza kupinganiwa na mtu ambaye haki zake za msingi zimekiukwa,” amesema

Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum Chadema amesema, “mabadiliko ya vifungu hivyo yanakiuka ibara za 26(2) ambayo inasema ‘kila mtu ana haki, kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria, kuchukua hatua za kisheria kuhakikisha hifadhi ya Katiba na sharia za nchi” sasa kwa kuwa Katiba haisemi mtu huyo lazima awe ameathirika na jambo hilo.”

“Ikiwa Bunge hili tukufu litapitisha mabadiliko ya vifungu hivyo, ni dhahiri kwamba vifungu hivyo vya sharia vitakuwa batili kwa kukinzana na Katiba, kwa sababu Kifungu cha 4(2) kinachopendekezwa kipo kinyume na Katiba na kinakinzana na Ibara za 26(2),” amesema

Makamba amesema, kila kiongozi wa umma anapoingia madarakani anaapa kuilinda Katiba pamoja na sharia.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Prof. Adelardus Kilangi

“Kiujumla, marekebisho haya yanapoka uhuru wa wananchi kufungua mashauri ya Katiba, mashauri yanayohusu haki za binadamu na hivyo kufunga milango ya mahakama kwa wananchi kudai haki zao za msingi,” amesema

Makamba amesema, marekebisho hayo yanapendekeza madai dhidi ya Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Spika, Jaji Mkuu na Naibu Spika yafunguliwe dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

“Marekebisho haya ni kinyume na msingi ya mgawanyo wa mamlaka baina ya mihimili mbalimbali katika nchi lakini tayari kuna maamuzi mbalimbali ya Mahakama ambayo yameshaamua kuwa Rais pamoja na viongozi wengine nao wanaweza kushtakiwa ikiwa watavunja Katiba,” amesema

Akisisitiza, Makamba amesema, “ni muhimu kwa wadaiwa kuhusishwa wao wenyewe na si kutenda makosa halafu akashtakiwa mtu mwingine ambaye ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali.”

“Pia, kwa kuweka kipingele hiki, inaondoa dhana nzima ya uwajibikaji na kiapo cha mhusika aliyeapa lazima awajibike kwa matendo yake,” ameongeza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!