Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mayweather kugharamia msiba wa Floyd
Kimataifa

Mayweather kugharamia msiba wa Floyd

Spread the love

FLOYD Mayweather, bondia anayeongoza kwa kulipwa fedha nyingi dunia, amesema atalipa gharama zote zitazohitajika katika msiba wa George Floyd. Inaripoti mtanzano wa BBC…(endelea).

Floyd, mmarekani mweusi aliuawa wiki iliyopita akiwa chini ya polisi wa Minneapolis. Kifo chake kimesababisha maandamano katika miji zaidi 80 nchini humo huku mauaji, uharibifu na uporaji vikishuhudiwa.

Taarifa za Mayweather kugharamia msiba wa Floyd zimethibitishwa na Leonard Ellerbe, Mtendaji Mkuu wake.

“Alionekana kama amechanganyikiwa kutokana na habari za kifo hicho, ni kweli ameahidi kulipa gharama zote za msiba wa Floyd,” amesema Ellerbe alipozungumza na mtandao wa ESPN.

Katika hatua nyingine, Umoja wa Ulaya (EU), umemuonya Donald Trump baada ya kauli yake kwamba, atatumia jeshi kukabiliana na ghasia.

EU imeeleza kwamba, hatua hiyo inaweza kuzidisha machafuko na kuwa na matokeo mabaya zaidi kuliko inavyotarajiwa.

Trump mapema leo mapema kwamba, iwapo magavana na mameya watashindwa kurejesha Amani kwenye maeneo yao, atalazimika kutumia jeshi.

“EU imeshtushwa na aina ya kifo cha Floyd, tena chini ya vikosi vya usalama. Haya ni matumizi mabaya ya madaraka,” amesema Josep Borrell, mkuu wa masuala ya kigeni na kuongeza “matumizi ya jeshi yanaweza kuwa na madhara zaidi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!