Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Takukuru nusura wamdake ‘mgombea’ ubunge CCM Ubungo, wanne mbaroni
Habari za SiasaTangulizi

Takukuru nusura wamdake ‘mgombea’ ubunge CCM Ubungo, wanne mbaroni

Spread the love

MWANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), anayejipanga kugombea ubunge katika Jimbo la Ubungo, jijini Dar es Salaam (jina tunalo), amewatoroka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Katika tukio hilo lililotokea jana jioni tarehe 31 Mei 2020, viongozi wanne wa chama hicho katika jimbo hilo, wanashikiliwa na Takukuru wilaya ya Ubungo.

Taarifa ambazo MwanaHALISI Online ilizopata leo Jumatatu tarehe 1 Juni, 2020 zinaeleza, viongozi hao wanatuhumiwa; kutoa rushwa na kuanza kampeni za uchaguzi mkuu Oktoba 2020 kabla ya wakati.

Msiri wa mtandao huu ameeleza, wakati wa mtego huo, mmoja kati yao alikurupuka na kukimbia na kutelekeza gari, kwenye tukio hilo viongozi wanne wamekamatwa.

“Walikuwa na mtu mmoja mmama anayetaka kugombea ubunge Ubungo, lakini yeye alikimbia ila akaacha gari na wenzake wanne ambao ni viongozi mbalimbali jimboni humo wakakamatwa na Takukuru wa Ubungo,” ameeleza.

MwanaHALISI Online limemtafuta Emmanuel Tarmo Boay, Kamanda wa Takukuru Wilaya ya Ubungo ili kupata ufafanuzi wake, amesema “suala hilo siwezi kulizungumzia mimi, atafutwe Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Kinondoni ambaye ndiye mzungumzaje wa mkoa.”

Pili Mwakasege, Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Kinondoni alipotafutwa, amesema suala hilo atalitolea ufafanuzi, “tutatoa taarifa rasmi. Tuko kazini.”

Endelea kufuatilia MwanaHALISI ONELINE kwa habari zaidi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

error: Content is protected !!