Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli amtumbua Dk. Ndugulile, amteua Dk. Mollel
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli amtumbua Dk. Ndugulile, amteua Dk. Mollel

Dk. Faustin Ndungulile
Spread the love

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemteua, Dk. Godwin Mollel kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea)

Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi tarehe 16 Mei, 2020 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema, uteuzi wa Dk. Mollel ambaye ni Mbunge wa Siha (CCM) unaanza leo.

Dk. Mollel anachukua nafasi ya Dk. Faustine Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni kupitia CCM ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Dk. Godwin Mollel

Dk. Ndugulile amekuwa naibu waziri wa wizara hiyo tangu tarehe 9 Oktoba, 2017 alipoapishwa na Rais Magufuli akichukua nafasi ya Dk. Hamisi Kigwangalla ambaye alipandishwa na kuwa waziri wa maliasili na utalii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

error: Content is protected !!