Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli amtumbua Dk. Ndugulile, amteua Dk. Mollel
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli amtumbua Dk. Ndugulile, amteua Dk. Mollel

Dk. Faustin Ndungulile
Spread the love

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemteua, Dk. Godwin Mollel kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea)

Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi tarehe 16 Mei, 2020 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema, uteuzi wa Dk. Mollel ambaye ni Mbunge wa Siha (CCM) unaanza leo.

Dk. Mollel anachukua nafasi ya Dk. Faustine Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni kupitia CCM ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Dk. Godwin Mollel

Dk. Ndugulile amekuwa naibu waziri wa wizara hiyo tangu tarehe 9 Oktoba, 2017 alipoapishwa na Rais Magufuli akichukua nafasi ya Dk. Hamisi Kigwangalla ambaye alipandishwa na kuwa waziri wa maliasili na utalii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

error: Content is protected !!