Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli ateua bosi mpya MSD
Habari za Siasa

Rais Magufuli ateua bosi mpya MSD

Spread the love

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemteua Brigedia Jenerali Dk. Gabriel Sauli Mhidize kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa iliyotolewa leo Jumapili tarehe 3, 2020 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema uteuzi wa Dk. Mhidize unaanza mara moja leo.

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Mhidize alikuwa Mkuu wa Hospitali ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Lugalo Jijini Dar es Salaam.

Brigedia Jenerali Mhidize anachukua nafasi ya Laurean Rugambwa Bwanakunu ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Bwanakunu ameongoza MSD tangu tarehe 23, 2015 baada ya kuteuliwa na Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete tarehe 6,2015.

Kabla ya uteuzi huo, Bwanakunu alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Ariel Glaser Paediatric AIDS Healthcare Initiative.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!