Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mazishi ya usiku yamshtua Zitto
Habari za Siasa

Mazishi ya usiku yamshtua Zitto

Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo
Spread the love

WAKATI Serikali ya Tanzania ikipiga marufuku utaratibu hasi wa mazishi ya usiku katika Halmashauri kadhaa nchini, Zitto Kabwe ameitaka serikali kutimiza wajibu wake. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Zitto ambaye ni Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini amesema, kwa sasa inashuhudiwa misiba mingi na watu kuzikwa usiku.

“Sitaki kuhisi kuna kitu kinafichwa. Nataka serikali itimize wajibu wake… Hivi sasa tuna shuhudia misiba mingi, mazishi ya watu usiku usiku na hata miili ya watu mitaani,” Zitto ameliambia Shirika la Habari la BBC.

Hata hivyo, serikali imepiga marufuku mazishi ya usiku, ikieleza watu wanaofariki kwa ugonjwa wa corona ama vinginevyo, wapewe heshima inayostahili.

“Katika kipindi hiki, tunaelekeza maofisa afya na waganga wakuu wa wilaya na mikoa, kuhakikisha familia zinashirikishwa kikamilifu na bila hofu au haraka katika kuandaa na kufanya mazishi kwa heshima zote za utu,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo iliyotolewa na Profesa Abel Makubi, Mganga Mkuu wa Serikali.

Kauli ya namna hiyo imewahi kutolewa na Job Ndugai, Spika wa Bunge kwamba, ni haki marehemu kuzikwa sehemu ambayo amilia yake imependa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!