Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Dawa ya corona kutua Tanzania
Habari Mchanganyiko

Dawa ya corona kutua Tanzania

Spread the love

DAWA ya ugonjwa wa corona (COVID-19), inayotengeneza nchini Madagascar, sasa itatumika nchini Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Ni kwa kuwa, Serikali ya Tanzania ina mpango wa kupeleka ndege yake nchini humo kwa ajili ya kubeba na kuleta nchini dawa hiyo, ili kutibu wananchi wake.

Rais John Magufuli ametoa kauli hiyo leo tarehe 3 Mei 2020, wakati akimwapisha Mwigulu Nchemba, Waziri wa Katiba na Sheria.

Mwigulu amechukua nafasi ya Balozi Dk. Augustine Mahiga aliyefariki dunia tarehe 1 Mei 2020 mjini Dodoma. Dk. Mahiga amezikwa jana nyumbani kwao Tosamaganga, Iringa. 

Rais Magufuli amesema,  Madagascar imeiandikia barua Tanzania kuhusu  dawa hiyo, na kwamba Tanzania imeona ni muhimu kuchukua dawa hiyo na kuileta nchini kwa ajili ya kuwasaidia Watanzania.

“Nimewasiliana na watu wa Madagascar, kuna dawa kule ya corona wanasema wameipata, nitatuma ndege hiyo dawa ije hapa tuitumie,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Songwe awafunda trafki kuzingatia uadilifu

Spread the loveASKARI wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Songwe wametakiwa kuendelea...

Habari Mchanganyiko

Mchimba madini jela maisha kwa kubaka, alihonga Sh 500

Spread the loveMahakama ya wilaya ya Songwe imemtia hatiani na kumhukumu kifungo...

Habari Mchanganyiko

Mlima wa Moto wazindua kongamano la SHILO kumuenzi Rwakatare

Spread the loveKANISA la Mlima wa Moto Mikocheni jijini Dar es Salaam,...

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

error: Content is protected !!