Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Dawa ya corona kutua Tanzania
Habari Mchanganyiko

Dawa ya corona kutua Tanzania

Spread the love

DAWA ya ugonjwa wa corona (COVID-19), inayotengeneza nchini Madagascar, sasa itatumika nchini Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Ni kwa kuwa, Serikali ya Tanzania ina mpango wa kupeleka ndege yake nchini humo kwa ajili ya kubeba na kuleta nchini dawa hiyo, ili kutibu wananchi wake.

Rais John Magufuli ametoa kauli hiyo leo tarehe 3 Mei 2020, wakati akimwapisha Mwigulu Nchemba, Waziri wa Katiba na Sheria.

Mwigulu amechukua nafasi ya Balozi Dk. Augustine Mahiga aliyefariki dunia tarehe 1 Mei 2020 mjini Dodoma. Dk. Mahiga amezikwa jana nyumbani kwao Tosamaganga, Iringa. 

Rais Magufuli amesema,  Madagascar imeiandikia barua Tanzania kuhusu  dawa hiyo, na kwamba Tanzania imeona ni muhimu kuchukua dawa hiyo na kuileta nchini kwa ajili ya kuwasaidia Watanzania.

“Nimewasiliana na watu wa Madagascar, kuna dawa kule ya corona wanasema wameipata, nitatuma ndege hiyo dawa ije hapa tuitumie,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!