Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Corona: Mbowe siku 14 karantini
AfyaHabari Mchanganyiko

Corona: Mbowe siku 14 karantini

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), sasa yupo karantini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Amechukua hatua hiyo yeye mwenyewe na familia yake. Ni baada ya mtoto wake Dudley kukutwa na maambukizi ya virusi vya corona (COVID-19). Kwa sasa Dudley anaendelea vizuri katika Hospitali ya Mwananyamala, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Clouds FM katika kipindi cha Jahazi tarehe 25 Machi 2020, Mbowe amesema, amejiweka karantini jijini Dodoma huku akiendelea na shughuli pia kuwasiliana na watu wake kupitia mtandao.

Amesema, amechukua hatua hiyo ikiwa hatua madhibiti kusambaa na kusubiri majibu, kwamba kama naye ana maambukizi hayo ama la “nasubiri majibu kujua kama nina maambukizi ama la.”

Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai, Kilimanjaro, amesema “unapokuwa na mgonja wa corona, jamii inakutazama kwa hofu na kwamba, kutokana na hivyo ni vema kujitenga kwa siku 14 huku nikisubiri majibu.”

Amesema, amekutana na watu wengi kabla ya kujiweka karantini, na kwamba ni jambo la kumuomba Mungu asiwe ameambukizwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

error: Content is protected !!