Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Mgonjwa wa kwanza wa corona Tanzania apona
Afya

Mgonjwa wa kwanza wa corona Tanzania apona

Isabela Mwampamba
Spread the love

ISABELA Mwampamba (46), mgonjwa wa kwanza kupatikana na virusi vya corona (COVID-19) nchini Tanzania, amepona na yupo huru kuungana na familia yake. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya amesema, muda wowote kuanzia sasa Isabela ataruhusiwa kuendelea na shughuli zake huku akitoa angalizo la kutonyanyapaliwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo tarehe 26 Machi 2020, Ummy amesema Isabela baada ya kupata vipimo vyote, vipimo vimeonesha kwamba yupo salama.

Tarehe 16 Machi 2020, Isabela alitangazwa kuwa mgonjwa wa kwanza kupatikana na virusi vya corona nchini, pia serikali ilianza ‘msako’ kwa wote  waliokuwa karibu na Isabela ili kuzuia kusambaa kwa ugonjwa huo.

Pia Ummy ameseama mpaka sasa, Tanzania ina jumla ya wagonjwa 13 ambapo kati yao wanane ni Watanzania na watano ni wageni na kwamba Arusha (2), Dar es Salaam (8),  Zanzibar (2) na  Kagera (1).

Amesema, wagonjwa 12 wote waliambukizwa nje ya nchi na mmoja aliambukizwa na mmojawao kati ya hao 12.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!