Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Corona: Mbowe siku 14 karantini
AfyaHabari Mchanganyiko

Corona: Mbowe siku 14 karantini

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), sasa yupo karantini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Amechukua hatua hiyo yeye mwenyewe na familia yake. Ni baada ya mtoto wake Dudley kukutwa na maambukizi ya virusi vya corona (COVID-19). Kwa sasa Dudley anaendelea vizuri katika Hospitali ya Mwananyamala, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Clouds FM katika kipindi cha Jahazi tarehe 25 Machi 2020, Mbowe amesema, amejiweka karantini jijini Dodoma huku akiendelea na shughuli pia kuwasiliana na watu wake kupitia mtandao.

Amesema, amechukua hatua hiyo ikiwa hatua madhibiti kusambaa na kusubiri majibu, kwamba kama naye ana maambukizi hayo ama la “nasubiri majibu kujua kama nina maambukizi ama la.”

Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai, Kilimanjaro, amesema “unapokuwa na mgonja wa corona, jamii inakutazama kwa hofu na kwamba, kutokana na hivyo ni vema kujitenga kwa siku 14 huku nikisubiri majibu.”

Amesema, amekutana na watu wengi kabla ya kujiweka karantini, na kwamba ni jambo la kumuomba Mungu asiwe ameambukizwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!