Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wapiga dili CCM kuhenyeshwa
Habari za SiasaTangulizi

Wapiga dili CCM kuhenyeshwa

Ofisi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Dodoma
Spread the love

ROBERT Mwinje (39) na  Nyemo Malendaa(20), wote makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Dodoma wanatarajiwa kupandishwa kizimbani muda wowote kutoka sasa. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mwinje aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Dodoma Mjini na Malendaa, mhudumu wa ofisi hiyo wanakabiliwa na makosa ya kula njama, kughushi na kuwasilisha nyaraka za uongo za uteuzi wa waombaji uongozi ndani ya chama hicho.

Sosthenes Kibwengo, Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mkoa wa Dodoma amesema Mwinje na Nyemo waligushi barua ya uteuzi wa waomba uongozi ndani ya chama hicho.

Pia walidai imetolewa na uongozi wa chama wilaya ya Dodoma, wakaikabidhi kwa mwanachama mmoja kwa hatua huku wakifahamu kwamba ni uongo.

Mwinje aliondolewa katika nafasi yake hiyo ya uenyekiti hivi karibuni na kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM kilichofanyika jijini Mwanza. Kikao hicho kiliongozwa na Dk.John Magufuli, Mwenyekiti wa chama Taifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!