Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Shitaka hili limemtibua Lema
Habari za SiasaTangulizi

Shitaka hili limemtibua Lema

Godbless Lema, Mbunge wa Arusha Mjini (katikati) akizungumza na waandishi muda mchache baada ya kutoka mahakamani mjini Singida
Spread the love

SHITAKA la kusababisha kuibua taharuki linalomkabili Godbless Lema, Mbunge wa Arusha Mjini, limemtibua. Anaripoti Mwandishi Wetu, Singida … (endelea).

Nje ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Singida, leo tarehe 25 Machi 2020, Lema ameonesha kushangazwa na shitaka hilo huku akihoji ‘nani aliyetaharuki?”

Lema amepandishwa kizimbani kwenye mahakama hiyo akikabiliwa na jumla ya mashtaka 15 likiwemo la kuibua taharuki kwa jamii.

Amepandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka hayo na mawakili upande wa Jamhuri, mbele ya Consolata Singano, Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo.

Mawakili hao wa serikali ni Michael Ng’hoboko, Monica Mbogo, Caren Malando na Rose Cholongola.

Katika mashtaka hayo, Lema anadaiwa kusababisha taharuki kwa jamii, kupotosha jamii. Anadaiwa kufanya makosa hayo tarehe 29 Februari 2020, akiwa mjini Manyoni mkoani Singida, kwenye mazishi ya kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Pia, anadaiwa kusambaza taarifa za uongo katika mitandao ya kijamii, zenye nia ya kupotosha jamii, kuhusu mauaji ya watu 14.

Hata hivyo, Lema ameachiwa kwa dhamana baada ya kukana mashtaka yote. Kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 15 Aprili 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

error: Content is protected !!