Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko TCRA yamburuza Idriss Sultan kizimbani
Habari Mchanganyiko

TCRA yamburuza Idriss Sultan kizimbani

Idriss Sultan
Spread the love

MSANII wa vichekesho Idriss Sultan, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi na wenzake wawili wakikabiliwa na kosa la kuchapisha maudhui mtandaoni bila kibali. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Washitakiwa wengine ni Daktari Ulimwengu na Isihaka Mwinyimvua.

Washtakiwa hao wamesomewa makosa yao mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi na Wakili wa Serikali, Batlida Mushi leo tarehe 20 Machi 2020.

Katika kesi hiyo namba 60 ya mwaka 2020, Wakili Mushi amedai kuwa Idriss na wenzake wametendeka kosa kati ya Machi 8, 2016 na Machi 12, 2020 katika maeneo tofauti jijini Dar es Salaam.

Inadaiwa katika maeneo hayo, walirusha maudhui kupitia chaneli ya YouTube huku wakiwa hawana kibali cha Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Baada ya kusomewa mashitaka hayo, washitakiwa wote wamekana, wameachiwa kwa masharti ya dhamana ya kuwa na mdhamini mmoja kwa kila mshitakiwa ambao wamesaini bondi ya Sh. 8 milioni kila mmoja.

Kesi imeahirishwa hadi tarehe 21 Aprili 2020 ambapo itarudi kwa ajili ya kusikilizwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

error: Content is protected !!