Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko TCRA yamburuza Idriss Sultan kizimbani
Habari Mchanganyiko

TCRA yamburuza Idriss Sultan kizimbani

Idriss Sultan
Spread the love

MSANII wa vichekesho Idriss Sultan, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi na wenzake wawili wakikabiliwa na kosa la kuchapisha maudhui mtandaoni bila kibali. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Washitakiwa wengine ni Daktari Ulimwengu na Isihaka Mwinyimvua.

Washtakiwa hao wamesomewa makosa yao mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi na Wakili wa Serikali, Batlida Mushi leo tarehe 20 Machi 2020.

Katika kesi hiyo namba 60 ya mwaka 2020, Wakili Mushi amedai kuwa Idriss na wenzake wametendeka kosa kati ya Machi 8, 2016 na Machi 12, 2020 katika maeneo tofauti jijini Dar es Salaam.

Inadaiwa katika maeneo hayo, walirusha maudhui kupitia chaneli ya YouTube huku wakiwa hawana kibali cha Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Baada ya kusomewa mashitaka hayo, washitakiwa wote wamekana, wameachiwa kwa masharti ya dhamana ya kuwa na mdhamini mmoja kwa kila mshitakiwa ambao wamesaini bondi ya Sh. 8 milioni kila mmoja.

Kesi imeahirishwa hadi tarehe 21 Aprili 2020 ambapo itarudi kwa ajili ya kusikilizwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!