Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Safu ‘nzuri ACT-Wazalendo
Habari za SiasaTangulizi

Safu ‘nzuri ACT-Wazalendo

Maalim Seif Shariff Hamad akikabishiwa kadi alipojiunga na ACT-Wazalendo
Spread the love

CHAMA cha ACT-Wazalendo kimepata viongozi wa juu wawili, walioridhiwa na wanachama wa chama hicho usiku wa manane kuamkia leo tarehe 15 Machi 2020. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam…(endelea).

Kwenye uchaguzi huo ulioana jana mchana tarehe 14 Machi 2020 na kumalizika saa 9 usiku, Maalim Seif Shariff Hamad amechaguliwa kuwa mwenyekti mpya wa chama hicho huku Zitto Kabwe, akiendelea kuwa kiongozi mkuu kwa mara ya pili.

Maalim Seif alipata kura amepata kura 337 sawa na asilimia 93.30 ambapo aliyemfuata Yeremia Kulwa Maganja amepata kura 20 swa na asilimia 5.55  huku Shilingushela Kahesa Nyangaki akipata kura 4 sawa na asilimia 1.01ambapo kura zilizoharibika zilikuwa mbili.

Kabla ya uenyekiti, Maalim Seif alikuwa Mshauri Mkuu wa wa chama hicho. Uchaguzi huo umeridhiwa na wajumbe wa mkutano huo kwamba ulikuwa huru, uwazi na haki.

Wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Omar Said Shabaan ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati Maalumu ya Uchaguzi wa ACT-Wazalendo amesema, jumla wajumbe walioshiriki mchakato huo ni 375, kura halali zilikuwa 367 na zilizoharibika nane.

“Kwa matokeo haya nikiwa mwenyekiti wa kamati maalumu ya uchaguzi namtangaza kwenu Maalim Seif kuwa mwenyekiti wa ACT -Wazalendo,” amesema Shabaan huku wajumbe wa mkutano huo wakishangilia.

Katika nafasi ya kiongozi mkuu wa chama hicho, Zitto amepata kura 276 sawa na asilimia 73.6 wakati Ismail Jussa amepata kura 91 sawa na asilimia 24.2.

Uchaguzi huo unaendelea leo katika nafasi mbalimbali ikiwemo Makamu Mwenyekiti, wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa na Kamati Kuu ya Chama ambapo kesho wajumbe watakaopatikana kesho watapiga kura ya kumchagua Katibu Mkuu wa chama na manaibu wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!