Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Safu ‘nzuri ACT-Wazalendo
Habari za SiasaTangulizi

Safu ‘nzuri ACT-Wazalendo

Maalim Seif Shariff Hamad akikabishiwa kadi alipojiunga na ACT-Wazalendo
Spread the love

CHAMA cha ACT-Wazalendo kimepata viongozi wa juu wawili, walioridhiwa na wanachama wa chama hicho usiku wa manane kuamkia leo tarehe 15 Machi 2020. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam…(endelea).

Kwenye uchaguzi huo ulioana jana mchana tarehe 14 Machi 2020 na kumalizika saa 9 usiku, Maalim Seif Shariff Hamad amechaguliwa kuwa mwenyekti mpya wa chama hicho huku Zitto Kabwe, akiendelea kuwa kiongozi mkuu kwa mara ya pili.

Maalim Seif alipata kura amepata kura 337 sawa na asilimia 93.30 ambapo aliyemfuata Yeremia Kulwa Maganja amepata kura 20 swa na asilimia 5.55  huku Shilingushela Kahesa Nyangaki akipata kura 4 sawa na asilimia 1.01ambapo kura zilizoharibika zilikuwa mbili.

Kabla ya uenyekiti, Maalim Seif alikuwa Mshauri Mkuu wa wa chama hicho. Uchaguzi huo umeridhiwa na wajumbe wa mkutano huo kwamba ulikuwa huru, uwazi na haki.

Wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Omar Said Shabaan ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati Maalumu ya Uchaguzi wa ACT-Wazalendo amesema, jumla wajumbe walioshiriki mchakato huo ni 375, kura halali zilikuwa 367 na zilizoharibika nane.

“Kwa matokeo haya nikiwa mwenyekiti wa kamati maalumu ya uchaguzi namtangaza kwenu Maalim Seif kuwa mwenyekiti wa ACT -Wazalendo,” amesema Shabaan huku wajumbe wa mkutano huo wakishangilia.

Katika nafasi ya kiongozi mkuu wa chama hicho, Zitto amepata kura 276 sawa na asilimia 73.6 wakati Ismail Jussa amepata kura 91 sawa na asilimia 24.2.

Uchaguzi huo unaendelea leo katika nafasi mbalimbali ikiwemo Makamu Mwenyekiti, wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa na Kamati Kuu ya Chama ambapo kesho wajumbe watakaopatikana kesho watapiga kura ya kumchagua Katibu Mkuu wa chama na manaibu wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!