Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kafulila ‘ainyea’ Chadema
Habari za SiasaTangulizi

Kafulila ‘ainyea’ Chadema

David Kafulila, Aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe
Spread the love

UZEMBE na kubebana ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ndio unakibomoa chama hicho kwa kiwango kikubwa. Anaripori Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

David Kafulila, Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe na mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini kupitia Chama cha NCCR-Mageuzi amesema, Chadema inateswa na umimi hivyo, kusababisha makada wake kukihama na kuingia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Uzembe na kubebana ndio siri ya wanasiasa wengi kuamua kuhama na kujiunga CCM. Haya ndio waliyakimbia CCM huko nyuma, sasa yanatokea Chadema,” ameeleza Kafulila na kuongeza;

“Kukimbilia CCM ni matokeo ya mapinduzi makubwa ya kimwenendo ndani ya CCM kama jina lake linavyosadifu. Uwezo mkubwa wa CCM chini  ya uenyekiti wa Rais Magufuli kutekeleza mkakati wa kujivua gamba la ufisadi. “

Kafulila ambaye aliwahi kuwa mwanachama wa Chadema na baadaye kutimkia NCCR Mageuzi na kushinda ubunge kupitia chama hicho mwaka 2010, amesema wanasiasa wa Chadema wamechoshwa na viongozi wao.

 “Watu wanaweza kwenda CCM kwa sababu wanavutiwa na CCM au wamechoshwa na upinzani. Kwa nionavyo mimi,  watu wengi wanajiunga CCM kwa kuvutiwa na CCM kutokana na ukarabati mkubwa wa CCM na Serikali yake uliofanywa na Rais Magufuli ndani ya muda mfupi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!