Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtatiro aagiza AMCOS Ruvuma vichunguzwe
Habari Mchanganyiko

Mtatiro aagiza AMCOS Ruvuma vichunguzwe

Julius Mtatiro, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru
Spread the love

JULIUS Mtatiro, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, ameagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), kuchunguza Vyama vya Ushirika vya Mazao (AMCOS), juu ya matumizi mabaya ya fedha za mauzo ya zao la korosho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Ruvuma … (endelea).

Mtatiro ametoa agizo hilo jana tarehe 20 Februari 2020, wakati akifungua mafunzo ya vyama hivyo na vyama vya akiba na mikopo, mkoani Ruvuma.

Kiongozi huyo wa wilaya ya Tunduru amedai kwmaba, kuna baadhi ya viongozi wa AMCOS wanatumia fedha za korosho kutoa rushwa, ili wapitishwe katika uchaguzi wa vyama hivyo, unaotarajia kufanyika hivi karibuni.

Mtatiro amedai kuwa, baada ya uchaguzi wa AMCOS kutangazwa, viongozi wa vyama hivyo wasio waadilifu, wameanza kupitisha fedha.

“Serikali iko makini, kwa uzoefu wangu nimeupata kwenye msimu huu wa korosho unanitosha kabisa kuanza kujua nini kinaendelea kwenye korosho. Umetangazwa uchaguzi watu wnaanza kupitisha hela kwenye AMCOS na nimeshawaambia TAKUKURU waanze kazi yao na tunawajua,” amedai Mtatiro na kuongeza:

“Ttunajua hela zinatoka wapi na katika uchaguzi watu ndio wanaanza kuweka hela kwenye AMCOS mimi sina maslahi kwenye korosho nitasimama upande wa wakulima viongozi na watendaji wanaotumia maadili kuhakikisha mazao haya yanaleta tija kwa wakulima.”

Mtatiro amewaonya vigogo wa AMCOS wanaoshiriki uchaguzi huo  kutofanya vitendo vya kuhujumu watu wengine wasishiriki uchaguzo huo.

“Zoezi la uchaguzi la mwaka huu ni makini sisi tunaratibu, tunajua wapi tutakukuta. Utakeleta choko choko sisi tutamshuhulikia, acheni watu wachukue fomu wao ambao hawataki kupumzika waache. Pangeni jichagueni peke yenu, pingeni wengine wasichukue fomu, kuna wengine wanasema nikitolewa kwenye AMCOS yangu hakutakalika, kusikalike? tuna njia nyingi tutakushughulikia,” ameonya Mtatiro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!