Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Meya Mbeya: Ushiriki wanasiasa, wananchi unahitajika
Habari za Siasa

Meya Mbeya: Ushiriki wanasiasa, wananchi unahitajika

David Mwashilindi, Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya (Chadema)
Spread the love

DAVID Mwashilindi, Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya (Chadema) amesema, katika kuhakikisha maendeleo yanawafikia wananchi, kunahitajika uwajibikaji wa pamoja kati ya wanasiasa na watumishi wa umma. Anaripoti Danson Kaijage, Da es Salaam…(endelea).

Mwashilindi ametoa kauli hiyo leo tarehe 19 Februari 2020, alipozungumza na waandishi wa habari jijini humo kuhusu mafanikio yaliyopatikana katika Jiji la Mbeya kwa kipindi cha miaka mitano sasa.

Amesema, Jiji la Mbeya limeweza kufanya shughuli za kuwapatia wananchi maendeleo kutokana na baraza la halmashauri ya jiji hilo, kwa kushirikiana vyema na watumishi wa umma kwa kila mmoja kisimamia majukumu yake.

Aidha ameeleza, kuwepo kwa vyama vya siasa ambavyo havifanani kwa mitazamo, kwamba haiwezi kuwa sababu ya kuzuia au kufanya maendeleo kuzorota.

Katika hatua nyingine Meya Mwashilindi amesema, kwa sasa Jiji la Mbeya limekuwa jiji la kwanza katika kujenga shule zenye mchepuo wa Lugha ya Kiingereza n ahata Waziri wa Tamisemi, Seleman Jafo kulipigia mfano.

Pamoja na kuwepo kwa shule za mchepuo wa Kiingereza amesema, kwa sasa Jiji la Mbeya limekuwa na urahisi wa kuingia na kutoka, kwani miundombinu hiyo imewezesha kuondokana na msongamano ambao ulikuwepo hapo awali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wizara ya Kilimo yapanga kutumia Sh. 1.2 trilioni 2024/25

Spread the loveWIZARA ya Kilimo, imepanga kutumia bajeti ya Sh. 1.2 trilioni...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

error: Content is protected !!