Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa UN waumizwa na uamuzi wa TZ
Habari za Siasa

UN waumizwa na uamuzi wa TZ

Balozi Augustine Mahiga, Waziri wa Katiba na Sheria
Spread the love

TUME ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa (UN), imeitoa wito kwa Serikali ya Tanzania kutathimini upya, uamuzi wake wa kuzuia asasi za kiraia na raia, kufungua kesi kwenye Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu (AfCHPR). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tume hiyo imetoa wito huo jana tarehe 3 Desemba 2019 kupitia ukurasa wake wa twitter.

Taarifa ya tume hiyo imeeleza kuwa, mahakama ni muhimu katika mchakato wa haki na uwajibikaji nchini Tanzania.

“Tumeumizwa na uamuzi wa serikali ya Tanzania kuzuia mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO’s), kupeleka kesi katika Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu.

Tunahimiza serikali kufikiria tena. Mahakama ni muhimu kwa haki na uwajibakaji nchini Tanzania,” inaeleza taarifa ya tume hiyo.

Madai ya Tanzania kutaka kujitoa katika mahakama hiyo yaliibuka hivi karibuni, na kupeleka Balozi Augustine Mahiga, Waziri wa Katiba na Sheria kutoa ufafanuzi wa suala hilo.

Katika ufafanuzi wake, Balozi Mahiga alisema Tanzania haijajitoa, bali imeomba kubadilisha itifaki kwenye mahakama hiyo, kwa madai kwamba inakinzana na sheria za Tanzania.

Balozi Mahiga alisisitiza kwamba, kama itifaki hiyo ambayo hakuihataja, haitarekebishwa, Tanzania itajitoa kwenye mahakama hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!