Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko OSHA kuwafikia wajasiriamali katika mazingira hatarishi
Habari Mchanganyiko

OSHA kuwafikia wajasiriamali katika mazingira hatarishi

Watengeneza batiki
Spread the love

WAKALA wa Usalama na Afya Mahala Pa Kazi (OSHA) umesema uko katika mkakati wa kuwafikia wajasiriamali, wanaofanya kazi katika mazingira hatarishi. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 2 Novemba 2019 jijini Dar es Salaam, Hadija Mwenda, Kaimu Mtendaji Mkuu OSHA, amesema wajasiriamali wengi wanafanya kazi katika mazingira hatarishi, kutokana na kutofikiwa na wakala huo.

Mwenda amesema OSHA ilishindwa kuwafikia wajasiriamali hao, kwa sababu ya kutosajiliwa, hali iliyosababishwa na kutokuwa na maeneo maalumu ya kufanyia kazi zao.

Kufuatia changamoto hiyo, Mwenda amesema OSHA imeanza utaratibu wa kuwafikia wajasiriamali hao, kwa lengo la kuwashauri namna ya kujikinga na mazingira hatarishi, kwenye mahala pa kazi.

Mwenda amesema hadi sasa OSHA imewafikia wajasiriamali 28,000 nchi nzima, na kwamba utaratibu huo ni endelevu ili kuhakikisha kundi hilo linafikiwa.

“Tuko kwenye mkakati wa namna ya kuwafikia wajasiriamali, sababu wanafanyakazi katika mazingira magumu na hatari. Mfano watengenezaji wa batiki hutumia kemikali hatari pasipo kuwa na elimu juu ya madhara yake na namna ya kujikinga,

Vvile vile mafundi gereji nao wako katika mazingira hatarishi. Hii yote ni kwa sababu hawajasiliwa. Inakuwa changamoto kuwajua walipo na namna ya kuwafikia,” amesema Mwenda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!