Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Baraza la Habari: Wanahabari waachwe huru
Habari MchanganyikoTangulizi

Baraza la Habari: Wanahabari waachwe huru

Spread the love

BARAZA la Habari Tanzania (MCT), limeitaka serikali kuhakikisha wanahabari wanatekeleza majukumu yao kwa uhuru. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Wito huo umetolewa na Kajubi Mukajanga, Katibu Mtendaji wa MCT, leo tarehe 2 Novemba 2019,  ikiwa ni maadhimisho ya siku ya kukomesha uonevu dhidi ya Wanahabari.

Taarifa ya baraza hilo inaeleza kuwa, wanahabari wakichwa huru na kutimiza majukumu yao bila hofu, wataisaidia serikali kutekeleza azma yake ya kupambana na ufisadi na matumizi mabaya ya fedha za umma.

“Pia watambue kuwa, bila kuwapo uandishi wa aina hiyo hakuna atakayebaki salama, maana waovu hawatakuwa na cha kuhofia na maliasili za taifa hazitabaki salama, kwani wahusika hawatakuwa na hofu ya kufichuliwa kwa wizi, ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka,” linaeleza tamko la MCT na kuongeza;

“Tunaamini wanahabari na vyombo vya habari vikiachwa vifanye kazi katika mazingira huru, bila kuwapo vitendo vya uonevu wataweza kuchangia vizuri katika azma ya serikali ya kupambana na ufisadi na matumizi mabaya ya fedha za umma.”

MCT imeeleza kuwa, wakati Tanzania inaadhimisha siku hiyo, wanahabari takribani 72 kutoka vyombo mbalimbali vya habari, wamekumbwa na mikasa wakati wakitimiza majukumu yao, katika kipindi cha mwaka mmoja kuanzia mwezi Oktoba 2018 hadi mwisho wa mwezi Oktoba 2019.

Baraza hilo limelaani ukiukwaji huo, na kueleza kwamba matukio ya wanahabari kupigwa, kunyang’anywa vifaa vyao vya kazi, kunyimwa taarifa, kukamatwa, kutishwa na kufungiwa kwa vyombo vyao, yamekuwa ni matukio ya kawaida, pasina wahusika kuchukuliwa hatua.

“Yapo matukio mengine mengi ya unyanyasaji dhidi ya wanahabari, na uingiliaji wa utendaji wa vyombo vya habari hapa nchini ambayo hayakuripotiwa rasmi na waathirika. Pia, yapo ambayo yaliripotiwa lakini hayakuwahi kuchunguzwa na vyombo vya dola na wala wahusika kuchukuliwa hatua,” imeeleza taarifa hiyo ya MCT.

Aidha, MCT imewataka wanahabari kuendelea kuripoti matukio yote ya ukiukwaji wa haki za wanahabari, pamoja na kufanya kazi zao kwa kuzingatia weledi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!