Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Upelelezi kesi ya Kabendera danadana
Habari za Siasa

Upelelezi kesi ya Kabendera danadana

Mwandishi Erick Kabendera akiwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Spread the love

UPANDE wa Mashtaka wa kesi inayomkabili mwandishi wa habari za uchunguzi nchini, Erick Kabendera, umedai bado upepelezi haujakamilisha. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Leo tarehe 24, Oktoba 2019, Wakili Mwandamizi wa Serikali Wankyo Simon mbele Hakimu Mkazi, Victoria Mwaikambo ameieleza mahakama kuwa shauri hilo lipo kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi haujakamilika. 

Upande wa utetezi umewakilishwa na Wakili Leonard Martin. Shauri hilo limeahirishwa hadi tarehe 7 Novemba, 2019.

Awali tarehe 11 Oktoba, mwaka huu, Wakili wa anayemtetea Kabendera, Jebra Kambole aliiarifu mahakama kuwa Kabendera anaomba kuzungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP), juu ya kuomba kusamehewa makosa yake.

Kabendera anashtakiwa Mahakamani hapo kwa makosa matatu ikiwemo kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kukwepa kodi kiasi cha Sh.173.3 milioni na utakatishaji fedha haramu kiasi cha Sh.173.3 milioni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!