Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Upelelezi kesi ya Kabendera danadana
Habari za Siasa

Upelelezi kesi ya Kabendera danadana

Mwandishi Erick Kabendera akiwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Spread the love

UPANDE wa Mashtaka wa kesi inayomkabili mwandishi wa habari za uchunguzi nchini, Erick Kabendera, umedai bado upepelezi haujakamilisha. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Leo tarehe 24, Oktoba 2019, Wakili Mwandamizi wa Serikali Wankyo Simon mbele Hakimu Mkazi, Victoria Mwaikambo ameieleza mahakama kuwa shauri hilo lipo kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi haujakamilika. 

Upande wa utetezi umewakilishwa na Wakili Leonard Martin. Shauri hilo limeahirishwa hadi tarehe 7 Novemba, 2019.

Awali tarehe 11 Oktoba, mwaka huu, Wakili wa anayemtetea Kabendera, Jebra Kambole aliiarifu mahakama kuwa Kabendera anaomba kuzungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP), juu ya kuomba kusamehewa makosa yake.

Kabendera anashtakiwa Mahakamani hapo kwa makosa matatu ikiwemo kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kukwepa kodi kiasi cha Sh.173.3 milioni na utakatishaji fedha haramu kiasi cha Sh.173.3 milioni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!