Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri wa JK afariki dunia
Habari Mchanganyiko

Waziri wa JK afariki dunia

Spread the love

OMARY Nundu, aliyewahi kuwa Mbunge wa Tanga Mjini na Waziri wa Uchukuzi katika Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Rais Jakaya Kikwete, amefariki dunia leo tarehe 11 Septemba 2019. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Taarifa ya kifo chake imetolewa na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), kitengo cha mawasiliano kwamba waziri huyo wa zamani, alifikishwa kwenye hospitali hiyo akiwa amefariki.

“Waziri wa zamani Mh.Omary Nundu alifikishwa leo MNH ,akitokea nyumbani kwa gari binafsi la wagonjwa akiwa tayari ameshafariki ,hivyo waliomleta waliamua wakahifadhi mwili wake katika Hospitali ya Rufaa ya Jeshi Lugalo,” imeeleza taarifa hiyo.

Nundu amefariki akiwa Mwenyekiti wa Bodi ya Airtel Tanzania baada ya kuteuliwa na Rais John Magufuli kushika nafasi hiyo tarehe 12 Juni 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!