Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri wa JK afariki dunia
Habari Mchanganyiko

Waziri wa JK afariki dunia

Spread the love

OMARY Nundu, aliyewahi kuwa Mbunge wa Tanga Mjini na Waziri wa Uchukuzi katika Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Rais Jakaya Kikwete, amefariki dunia leo tarehe 11 Septemba 2019. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Taarifa ya kifo chake imetolewa na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), kitengo cha mawasiliano kwamba waziri huyo wa zamani, alifikishwa kwenye hospitali hiyo akiwa amefariki.

“Waziri wa zamani Mh.Omary Nundu alifikishwa leo MNH ,akitokea nyumbani kwa gari binafsi la wagonjwa akiwa tayari ameshafariki ,hivyo waliomleta waliamua wakahifadhi mwili wake katika Hospitali ya Rufaa ya Jeshi Lugalo,” imeeleza taarifa hiyo.

Nundu amefariki akiwa Mwenyekiti wa Bodi ya Airtel Tanzania baada ya kuteuliwa na Rais John Magufuli kushika nafasi hiyo tarehe 12 Juni 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!